Skip to main content

UWANJA ITAKAPOPIGWA FAINAL YA UEFA(CARDIFF) KUZIBWA KWA JUU KUHOFIA MAGAIDI.!

Bado tu tukio lililotokea Ujerumani la bomu kulipuka karibia na basi la klabu ya Borussia Dortmund linaitesa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA.

Sasa kuelekea katika mchezo wa fainali ya Uefa Champions league utakaopigwa mwezi june kati uwanja Principality Stadium, 
 kumekuwa na hofu kwamba magaidi wanaweza kutumia ndege ndogo za kurusha(drones) kushambulia uwanja huo.

Maofisa wa UEFA wamefanya vikao vya siri na maofisa wa usalama wa Wales na wa uwanja huo ili kujaribu kutafuta mbinu sahihi ambayo itasaidi kudhibiti jambo hilo lisitokee wakati wa fainali hiyo.

UEFA wameanza kufikiria kuuziba uwanja huo kwa juu ili vitu kama drones visiweze kupenya katika uwanja huo kupitia juu, suala ambalo tayari wamiliki wa uwanja huo wameanza kulifanyia kazi.

Fainali hiyo itakayopigwa tarehe 3 June inatarajia kuvuta watu mbali mbali katika kila kona ya dunia, 
huku uwanja huo utaweza kubeba watu 75,000 na ujio wa watu wengi siku hiyo inaweza kuwavutia magaidi suala ambalo UEFA wameanza kulihofia.

Inasemekana zaidi ya askari 14,000 tayari wamejipanga kufanya kazi ya ulinzi siku hiyo, huku pia kukianza kufungwa vifaa maalum karibia na uwanja huo ambavyo vitaweza kugundua vitu vya mlipuko.

Kundi la kigaidi la IS(Islamic State) ndio limekuwa likileta hofu kubwa katika soka kwani hata mlipuko uliotokea Dortmund polisi wamekiri kuwa mlipuaji alikuwa mzoefu sana,
 na kundi hilo ndio limekuwa likitumia drones mara nyingi katika matukio yao.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...