Skip to main content

HII KALI;MKE NA MUME KUTOKA KENYA WAHINDA MBIO ZA PARIS MARATHON.!

Mkenya Paul Lonyangata alipata ushindi mkubwa wa saa 2 dakika 6 na sekunde 10 katika historia yake licha ya kupoteza muda bora.

Mpinzani wake pia kutoka Kenya katika mbio hizo Stephen Chebogut alikuwa wa pili kwa muda wa saa 2 dakika 6 na sekunde 56 huku Solomon Yego pia wa Kenya akishikilia nafasi ya tatu katika muda wa saa 2 dakika 7 na sekunde 13.

''Nahisi vyema sasa kwa sababu lengo langu lilikuwa kuja hapa na kuibuka mshindi '',alisema.

Huku Paris ikiwa na jua Rionoripo ambaye ni mkewe mshindi wa mbio hizo upande wa wanaume Paul Lonyangata aliibuka mshindi.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 23 aliweka muda bora wa saa 2 dakika 20 na sekunde 50 na hivyobasi kushinda muda wake binafsi aliouweka kwa zaidi ya dakika 4. 

Ushindi wa wanandoa hao ulirudisha tabasamu kwa wanariadha Wakenya baada ya habari za kushangaza kwamba bingwa wa mbio za marathon za Olimpiki upande wa wanawake Jemima Sumgong alipatikana ametumia dawa za kusisimua misuli.

Sumgong ni Mkenya wa kwanza mwanamke kushinda medali ya Olimpiki katika mbio za marathon alipoibuka mshindi katika michezo ya Olimpiki ya Rio.

Mwanariadha huyo ambaye pia ni bingwa mtetezi wa mbio za london Marathon alipatikana alitumia dawa aina ya EPO baada ya kufanyiwa uchunguzi na IAAF.

Lonyangata mwenye umri wa miaka 24 aliamua kuongeza kasi baada ya kilomita 35 akampita Chebogut na hivyobasi kujiongezea mataji aliyoshinda katika mbio za Shanghai marathon 2015 pamoja na Lisbon miaka miwili mapema.

Katika mbio za wanawake Rionoripo alifuatwa kwa karibu na Mkenya mwenzake Agnes Barsosio kwa kuweka muda wa saa 2 dakika 21 na sekunde 02 huku Flomena Cheyech akimaliza udhia.

Rionoripo alivunja rekodi iliokuwa imewekwa na raia wa Ethiopia Feyse Tadese ya saa 2 dakika 21 na sekunde 06 mwaka 2013.BBC

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...