Skip to main content

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani.

Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.
 Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine.

7: Rand – Afrika Kusini (1$=14)
Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa,
thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14.

6: Pula – Botswana (1$ = 10.8)
Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokanayo na uchimbaji wa madini na ufugaji. Dola moja huuzwa kwa Pula 10.8.

5: Dihram – Morocco (1$=9.9)
Morocco ni moja kati ya nchi ambazo zinajivunia kuwa na fedha yenye thamani barani Afrika ambapo uchumi wake unatokana na kujijenga kwa sekta za Utalii, Viwanda na Kilimo. Dola moja ni sawa na Dihram 9.9.

4: Kwacha – Zambia (1$ = 9.84)
Kwacha ni moja kati ya sarafu maarufu sana Kusini mwa Afrika ambayo hutumika nchini Zambia.

 Sarafu ya Kwacha imekuwa na nguvu sana na thamani kutokana na uchumi mkubwa wa nchi hiyo unaotokana na mapato katika sekta ya Utalii. Dola moja ina thamani ya Kwacha 9.84.

3: Pound – Sudan (1$=6.4)
Licha ya kuwa katika vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu lakini Sudan imendelea kuifanya sarafu yake kuwa na thamani na yenye nguvu zaidi katika kipindi cha miaka mingi kutokana na uchimbaji wa mafuta ambayo yanauzwa nje ya nchi, Uvuvi, na Kilimo ambavyo ni vyanzo vya mapato ya nchi. Dola moja hununuliwa kwa Pound 6.4 za Sudan.

2: Cedic – Ghana (1$= 4)
Ghana ndiyo nchi pekee ambayo imeingia kwenye list ya nchi zenye sarafu yenye thamani na nguvu kubwa Afrika kwa upande wa nchi za Afrika Magharibi ikikamata nafasi ya pili. 

Hivi karibuni nchi hiyo imegundua mafuta hivyo kuwaongezea mapato zaidi bila kujali kama bidhaa zao zimeshuka kwenye mauzo. 
Nchi hiyo inajivunia kuwa na Demokrasia imara barani Afrika hivyo imejiimrisha vizuri katika uchumi. Dola moja hununuliwa kwa Cedic 4.

1: Dinar – Libya (1$= 1.4116)
Dinar ambayo ni fedha ya Libya inakamata nafasi ya kwanza kwa kuwa fedha yenye thamani na nguvu kubwa barani Afrika ambapo Dola moja hubadilishwa kwa Dinar 1.4116.


Comments

Popular posts from this blog

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...