Skip to main content

Upangaji Matokeo Hispania. Kocha na Mtendaji wa Eldense Waishutumu Barcelona..!

Kocha wa klabu ya Eldense, Filippo Vito di Pierro na mkurugenzi mtendaji wa klabu hiyo Nobile Capuani wamekataa kuwa walihusika na shutuma ambazo zimewekwa dhidi yao kuhusiana na upangaji matokeo huku wakilaumu klabu ya Barcelona B kwa kukataa kuacha kufunga walipopoteza kwa mabao12-0.

Watu hawa wawili walikuwa miongoni mwa watu watano ambao walikamatwa na polisi wa usalama wa raia na makosa ya jinai huko Hispania baada ya matokeo hayo mabovu ya daraja la tatu.
Waliachiwa siku ya Jumatano lakini wana kesi za kujibu dhidi yao ambazo zinahusu rushwa baina ya watu na kujihusisha na makundi ya kihalifu.

Akihojiwa kuhusiana na tuhuma hizi na kama kwa namna yoyote wamehusika na wanafahamu lilitokea kwenye upande wa Eldense na upangaji matokeo, Di Pierro alisema “hakuna ukweli wowote na haijatokea.”
“Baada ya udhalilishaji huo kutokana na matokeo ya siku ya Jumamosi naamini kuwa wachezaji wetu wote 20 ni wasafi katika hili.”
“Wachezaji wa Barcelona hawakuheshimu kanuni ya utu na busara baiana ya timu hizi. Kiukweli wachezaji wetu katika benchi waliomba Barcelona isiendelee kufunga na wachezaji wa Barcelona waliweza kujibu kwa kusema tu “Samahani hatuwezi kuacha.”

Akikataa kujihusisha na suala lolote la upangaji matokeo, alisema: “Hii ni moja tu ya zile ndoto mbaya.
“Sielewi wanazungumzia nini kwakweli, sio sehemu ya nilivyo na sipo hivyo. Nitakuwepo kusaidia vyombo na mamlaka husika kwa namna yoyote nitakayoweza.”

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...