Skip to main content

Sababu 3 kwanini Davido ana mzuka na collabo yake na Joh Makini.! Bofya picha hii kujua zaidi

April 3, 2017, Davido pia alipost picha Instagram inayoonesha kuwa wawili hao wameshoot video ya collabo yao.

Kwa kila namna, inaonesha kuwa Davido anaikubali sana ngoma hii aliyoshirikishwa na Mwamba wa Kaskizini kiasi cha mara zote kuwa wa kwanza kutoa updates. Hizo, ni dalili njema kuwa wimbo huu utakuwa mkubwa Afrika. 

Hii inakuwa collabo yake ya pili kushirikishwa na msanii toka Afrika Mashariki baada ya Number One ya Diamond. Swali ni, kwanini staa huyo wa Nigeria ameonesha kuwa na mzuka na project hizi ?

1. Davido ni shabiki mkubwa wa Joh Makini
Kabla ya hata kutweet kuhusu collabo yao, Davido aliwahi kusema wazi kuupenda wimbo Nusu Nusu wa Joh Makini. Ni wazi kuwa amekuwa akipenda ngoma za Joh kwa muda na ndio maana ilikuwa rahisi kuirukia ngoma ya Joh.

2. Davido anajua anavyokubalika Tanzania (Afrika Mashariki)
Tangu ashirikishwe na Diamond kwenye Number One, Tanzania imekuwa katika mahali special moyoni mwa Davido.
        Pamoja na kwamba kuliwahi kutokea uhasama kati yake na mashabiki wa muziki Bongo kutokana na kauli yake ya ‘And they steal again’ baada ya Idris Sultan kushinda shindano la Big Brother Africa, yote yalipita na upendo ukarudi sehemu yake.

 Hadi sasa Davido ni jina lenye uzito mkubwa Bongo na pia idadi kubwa ya followers wake kwenye mitandao ya kijamii hasa Instagram, ukitoa Nigeria, ipo Tanzania

3. Ngoma ni kali

Mimi nimepata bahati ya kuisikia ngoma hii. Naelewa kwanini Davido ameipania, ni kali sana. Naamini itamfikisha Joh Makini kwenye level za juu zaidi Afrika.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...