Skip to main content

WANAFUZI KATIKA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NAUTANGAZAJI{A.J.T.C}ARUSHA KUFANYA MAHAFALI YA KUMALIZA CHUO......//

 17,November,2016.
Wanafunzi wanaomaliza masomo katika Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji{ARUSHA JOURNALISM TRAINIG COLLEGE}wanatarajia kufanya mahafali ya kumi namoja{11} kwa chuo hicho ikiwa nipamoja nakuwaaga wanafunzi hao  chuoni hapo wakiwa wanamliza masomo yao kwa ngazi ya stahahada kama ilivyokawaida ya kila mwaka kwa chuo hicho.


Mahafali hiyo ambayo itafanyika katika viwanja vya PPS maeneo ya JR. MBAUDA  natayari maandalizi yakutosha kuelekea hafla hiyo kubwa yameanza kufanyika kikamilifu zaidi.

Akizungumza katika eneo la ukumbi wa uwasilishwaji wa vipindi vya radio na television katika chuo hicho mmoja wa wakufunzi chuoni hapo Mwalim ONESMO ELIA MBISE{pichani}amesema wanafunzi hawana budi kufuata sharia za chuo hicho.

Unapokuwa chuoni unapaswa kutambua wajibu wako kama mwanafunzi ikiwa ni pamoja na kuhudhuria hapa katika eneo hili lakini pia kuhudhuria madarasaniAliongeza nakusema Mwalim huyo baada ya tetesi kuzagaa kwa wanafunzi wengi chuoni hapo  wakidai kuwa kesho ijumaa itakuwa hasa nisiku ya maandalizi{namasomo yatakuwa haba jambo ambalo si kweli} kuelekea hafla hiyo kubwa ambayo hufanyika kila mwishoni mwa mwaka.


Mahafali hiyo inatarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi November 2016 siku ya Jumamosi ,licha ya uongozi wa chuo hicho kutoa mualiko kwa watu wote bila kuchagua rangi wala kabila katika kuhudhuria mahafali hiyo adhim bila kukosa.



Hata hivyo makam mkuu wa chuo hicho Bwana ANDREW NGOBOLE nae ameweza kuzungumzia hilo  kwa nafasi yake nakusema kuwa idadi ya wanafunzi wanaotarajia kumaliza chuo kuelekea hafla hiyo nzito kwa mwaka huu imepungua mpaka kufikia thelathini nambili{32} ambayo ni dadi ndogo tofauti namiaka mingine ambayo ilikuwa zaidi na idadi hiyo tajwa. 
Imeandaliwa na SWALHA H. JUMA Kutoka chuo cha Uandishi wa habari na utangazaji{Arusha Journalism Training College}.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...