Skip to main content

MICHANGO MAAFA YA KAGERA YAFIKIA BILIONI 5.4 ................//

Kamati ya maafa ya mkoa wa Kagera imeishapokea zaidi ya shilingi Bilioni 5.4 hadi kufikia Novemba 10, mwaka huu ambayo ni michango ya wadau mbalimbali ambao ni pamoja na taasisi binafsi na zile za kiserikali, mashirika ya kimaifa,nchi marafiki inatotolewa kwa lengo la kukabili maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea mkoani humo na kusababisha madhara makubwa.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mstapha Kijuu mbele ya waandishi wa habari wakati akielezea juhudi za kamati hiyo katika kukabiliana na madhara ya tetemeko,

amesema kamati hiyo imeishatumia kiasi cha shilingi bilioni 1.1 kutokana na michango hiyo kwa ajili kukarabati miundombinu ambayo imeharibiwa na tetemeko ambayo ni pamoja na zahanati,vituo vya afya,shule za msingi na sekondari.

tetemeko-la-ardhinyumba-tetemeko_640_392

Aidha,mkuu huyo wa mkoa pamoja na kuwapongeza waliochukua hatua ya kujenga upya nyumba zao ziliharibiwa na tetemeko,amesema kamati ya maafa ya mkoa wa Kagera iko kwenye mchakato wa kuhakikisha makundi maalumu yenye uhitaji yanarejesha katika hali ya kawaida miundombinu ya nyumba zao za makazi iliyoharibiwa na tetemeko,

amesema kamati hiyo tayari imeishafanya makubaliano na Kanisa la Pentekoste ambalo limeahidi kujenga nyumba za wenye uhitaji kwa awamu mbalimbali ambapo katika awamu ya kwanza kanisa hilo litajenga nyumba 370.

Nao baadhi ya wazee na wajane wameonyesha kutoridhishwa na utaratibu unaotumika wa kuyabainisha makundi yenye uhitaji,wakizungumza wamesema utaratibu wa kuyabaini makundi hayo kuwa unawabagua baadhi ya waathirika wa tetemeko wenye uhitaji.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...