Skip to main content

Sunday, 20 November 2016.MAHAFALI YA KUMI NAMOJA KATIKA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI|Arusha Journalism Training college|..

   Wanafunzi katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha|Arusha journalism trainig college| wametakiwa kukabiliana na changamoto za ajira nchini ikiwemo sheria iliyopitishwa na      wabunge kwa waandishi wa habari.
 

Hayo yamesemwa na meya wa jiji la Arusha Bwana Kalist Lazaro wakati akiwatunuku vyeti wahitimu wa chuo hicho katika mahafali ya kumi na moja yaliyofanyika mapema jana katika ukumbi wa PPS maeneo ya JR Mbauda jijini hapa.

 Meya huyo amesema  kuwa  waandishi wa habari wanatakakiwa kuungana na kuwa kitu kimoja ili kuweza kupaza sauti zao wakiwa kama vioo vya jamii  kuitaka serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania juu ya kuwataka wabunge nawao kuongeza viwango vya elimu zao.


.

meya lazaro amewataka wazazi na walezi kutokata tamaa kwa kuwaendeleza watoto wao kwa ngazi nyingine ya kimasomo ila waweze kuwa bora zaidi na kuweza kukabiliana na soko la ajira kwa sasa kitaifa na kimataifa.

Hata hivyo ameongeza kwa kuwataka wahitimu wa ngazi hiyo ya stashada kutokuishia hapo na kuweza kuongeza viwango vya elimu ikiwemo elimu ya degree kama ambavyo wamevyotakiwa na sheria hiyo ili kuweza kupmbana na soko la ajira.                                     


 Aidha wahitimu hao wamewashukuru walimu,uongozi wa chuo , wazazi pamoja na wanafunzi wenzao kwa kuwa pamoja nao kwa kipindi chote cha masomo.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...