Skip to main content

Friday, November 18, 2016 Daktari FEKI anaswa Hospitali ya Rufaa Dodoma.............//

Mkazi wa Area C mjini hapa, Boniface Kigomba amekamatwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma akiwa katika harakati za kuwaonyesha wagonjwa kliniki ya wajawazito. 

Tukio hilo lilitokea jana na kusababisha wagonjwa, madaktari na wauguzi kukusanyika katika ofisi ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo kumshuhudia. 

Hata hivyo, Polisi aliyekuwa amevalia kiraia alifika hospitalini hapo saa 8:00 mchana na kumfunga pingu Kigomba na kumpeleka kituoni. 

Kigomba alikamatwa akiwa na kitambulisho cha uanafunzi cha Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) chenye namba za usajili T/DOM/2014, muhuri wa hospitali hiyo na kitambulisho kinachoonyesha ni muajiriwa wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF. 

Vitambulisho vingine alivyokutwa navyo ni cha mpigakura, uanachama wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na karatasi zilizokuwa zimeandikwa gharama za matibabu. 

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Caroline Damian alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakipata malalamiko kutoka kwa wagonjwa juu ya ukiukwaji wa maadili unaofanywa na mmoja wa madaktari hospitalini hapo. 

“Tulimuwekea mtego siku nyingi lakini leo (jana) tuliambiwa ameonekana akiwa eneo hili ndipo tulipomkamata na kumhoji na ameonekana hakuna anachokijua kuhusiana na taaluma ya udaktari ingawa alisema yeye ni mwanafunzi wa udaktari Udom,” alisema. 

Dk Caroline alisema Kagomba alipohojiwa alidai kuwa alikuwa akiwaelekeza wagonjwa eneo zinakotolewa huduma hospitalini hapo. 

Alisema mbali na wagonjwa kutapeliwa fedha, hivi karibuni kumekuwa na matukio ya wizi wa vifaa. 

Mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE), Tawi la Dodoma, Pafect Kadawele ambaye anaishi naye katika nyumba ya wazazi wake Area C, alisema alikutana na Kigomba miaka miwili iliyopita katika Kanisa la Upendo na baada ya kumueleza kuwa hana mahali pa kuishi aliamua kumchukua na kuishi naye. 

Alisema kila siku amekuwa akimueleza kuwa anakwenda Udom anakosomea shahada ya udaktari. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema wameanza kushughulikia tatizo hilo na atatoa taarifa leo. 

Makamu Mkuu wa Udom, Profesa Idrisa Kikula alisema katika orodha ya wanafunzi chuoni hapo hakuna jina linalofanana na la Kagomba. 

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...