Skip to main content

Yanga imeshindwa kusonga mbele michuano ya mabingwa Afrika..!!

Dakika 90 za mchezo wa marudiano wa klabu bingwa Afrika kati ya Zanaco FC dhidi ya Yanga zimemalizika bila timu hizo kufungana na moja kwa moja Yanga imetupwa nje ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya vilabu.


 Yanga imehukumiwa baada ya kuruhusu kufungwa goli kwenye uwanja wake wa nyumbani ambapo ililazimishwa sare ya goli 1-1 kwenye uwanja wa Taifa Jumamosi iliyopita.

 Matokeo hayo yanaifanya Yanga kuangukia kwenye michuano ya Confederation Cup na kuiacha Zanaco ikifuzu katika hatua ya makundi ya Caf Champions League 2017.

 Msimu uliopita Yanga ikiwa chini ya Hans van der Pluijm, ilifuzu hatua ya makundi ya michuano ya Confederation Cup baada ya kuondoshwa kwenye michuano ya Caf Champions League.

 Yanga ilihitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya kuanzia magoli 2-2 ili isonge mbele kwenye hatua inayofata lakini imeshindwa kufanya hivyo na kujikuta ikiondoshwa kwenye michuano hiyo baada ya sare tasa kwenye mechi ya marudiano.


Zanaco wamefaidika na goli la ugenini walilopata kwenye mechi yao ya jijini Dar es Salaam na kuizuia Yanga kupata goli kwenye ardhi ya Zambia.

 Kesho Jumapili March 19, 2017 wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya kombe la shirikisho Afrika Azam FC itakuwa ugenini Swazland ikicheza mechi ya marudiano dhidi ya Mbabane Swallows. 

Mechi ya kwanza kwenye uwanja wa Azam Complex Azam ilipata ushindi wa goli 1-0.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...