Skip to main content

Hawa hawajafungwa kwao msimu huu.!

Ukiacha Juventus ambaye hadi sasa katika michezo 33 hakuna mechi waliyopigwa, kuna timu ambazo msimu huu hawajapoteza mchezo hata mmoja wa ligi katika uwanja wao wa nyumbani.

1.Tottenham Hotspur.
Katika msimu huu wa ligi hadi sasa Tottenham wameshacheza michezo 14 katika uwanja wao wa nyumbani wa White Hart Lane.
 
Hakuna timu ambayo imetembelea uwanja huo na kuondoka na alama zote 3,Hart Lane pamekuwa pagumu sana kwa wapinzani kwani kati ya mechi hizo 14 walizocheza wameshinda michezo 12 na kutoka suluhu miwili.Tottenham kwa ujumla msimu huu wamefunga magoli 33 na kufungwa 7 tu,wanatafuta ubingwa wao wa kwanza tangia mwaka 1961.
 
2.Real Madrid.
Madrid msimu huu pamoja na kwamba kuna kipindi walikuwa wakipatwa na matokeo yasiyoeleweka lakini nao hawajawahi kifungwa nyumbani. Katika ligi yao ya nyumbani Real Madrid msimu huu wamepoteza michezo miwili tu dhidi ya majirani zao Athletico na ule dhidi ya Sevilla.
 
 Lakini hawajawahi kufungwa wakiwa Santiago Bernabeu kwani michezo yao 14 waliyocheza uwanjani hapo wameshinda michezo 11 na kusulu michezo mitatu, na wakiwa wamefunga magoli 36.
 
3.Juventus.
Uwanja wa nyumbani wa Juventus umekuwa kama Jehannam kwa timu zinazoenda kupatembelea msimu huu. Katika ligi ya Italia hakuna timu ambayo imeambulia alama hata moja katika uwanja huo. Juventus wamechukua alama zote 45 katika michezo 15 waliyocheza uwanjani hapo, na ni kati ya viwanja vigumu sana kucheza dhidi yao. 
 
Si hivyo tu bali katika michezo 33 kwa ujumla ya Juventus hawajapoteza mchezo hata mmoja.
 
4.Bayern Munich.
Allianz Arena napo ni pagumu, uwanja huo wa nyumbani wa Bayern Munich hawajawahi kuangusha alama 3 katika uwanja huo. Hadi sasa katika ligi yao ya nyumbani Bayer Munich wameshacheza michezo 12 katika uwanja huo, kati ya michezo hiyo wameshinda mara 9 huku wakitoka sare mara 3 na kupata jumla ya magoli 38.Fc Koln,Hoffeinheim na Schalke 04 ndio timu pekee zilizogawana alama na Bayern katika uwanja huo.
 
5.Borussia Dortmund.
Wapinzani wakubwa wa Bayern Munich katika ligi ya Ujerumani, Dortmund nao wakiwa Westfalenstadion hawajapoteza mchezo hata mmoja. Wameshacheza michezo 11 uwanjani hapo na katila michezo hiyo wameshinda mara 8 huku wakitoka suluhu mara tatu na kufunga jumla ya magoli 28.
 
6.PSG.
Miamba ya Ufaransa, wakiwa nyumbani kwao wameshinda kwa wastani wa 64% na zilizobaki wametoa suluhu. Michezo 14 waliyocheza wamepata suluhu michezo 5 huku wakishinda michezo 9 kwa idadi ya magoli 28, wakiwa nyumbani kwao wameruhusu nyavu zao kutikiswa mara 5 tu.


Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...