Skip to main content

Hizi ni sababu 10 kwanini Kante anapendwa na kila mtu.!

1.Amekuwa nyota kwa kila timu aliyochezea.Toka alipokuwa Leicester City mchango wake ulikuwa mkubwa sana na kuisaidia Leicester kubeba ubingwa.Amehamia Chelsea nako ni vivyo hivyo kwanj amewaweka uongozi wa ligi na amekuwa muhimu sana kwao.

2.Hana makuu.Kante ni mchezaji ambaye nje ya uwanja utamuona mshamba mshamba,hana mbwembwe za misuko sijui style za nywele,na anasema yeye baada ya mechi tu hurudi nyumbani kulala.
 
3.Alivyokuwa mhimili wa Leicester.Kwa timu ya Leicester kuchukua ubingwa wa Uingereza ilikuwa ndoto.Hii ni sababu ambayo kila timu inatamani kuwa na Kante wao,na ndio maana wakati wa usajili timu mbali mbali zilimpigania Kante.
 
4.Tabasamu lake.Kante ni mchezaji ambaye ni ngumu sana kukasirika na muda wote anaonekana na furaha.Wataalamu wa mambo ya soka wanasema kati ya kitu ambacho mashabiki wengi wanachofurahi kwa Kante tabsamu ni mojawapo.
 
5.Bado anakumbuka alipotoka.Baada ya kutoka Leicester City wengi walidhani ndio mwisho wa Kante na Leicester,lakini Kante bado ana mapenzi na Leicester.Katika ushindi wao dhidi ya Sevilla, Kante alikuwepo kuwashangilia Leicester wakitinga robo fainali ya UEFA.
 
6.Hakumsaliti Ranieri.Kabla ya kocha aliyewapa ubingwa Leicester City, Claudio Ranieri kutimuliwa kulikuwa na habari kwamba wachezaji wakubwa walimsaliti. Ryad Mahrez na Jamie Vardy ninmiongoni mwa majina makubwa ya wasaliti wa Ranieri. Lakini Ngolo Kante alikuwa swahiba wa Ranieri na hata katika mchezo kati ya Chelsea na Leicester City walionekana kufurahi pamoja.
 
7.Yeye utamuona tu uwanjani.Kante ni mtu ambaye hata shopping huwa haonekani sana. Muda wake mwingi huutumia nyumbani akitoka nyumbani ni mazoezini akitoka mazoezini ndani kupumzika.
 
8.Hakuwa gumzo miaka miwili iliyopita.Ni kama zero to hero,miaka miwili iliyopita hakuna mtu ambaye alikuwa akimzungumzia Kante. Miaka hiyo Kante alikuwa Cannas hakuwa na jina na hata kwenye Social medias lakini sasa yuko mdomoni mwa kila mtu.
 
9.Sio bishoo.Katika umri wake ni dhahiri kwamba alitakiwa awe bishoo kama Ozil,Pogba au Depay.Lakini Kante sio bishoo hata kidogo, ukimuangalia maisha yake utagundua anaishi kama mzee wakati yeye ni kijana.
 
10.Siku zinavyozidi kwenda ndiyo anakuwa gumzo.Wengine walidhani baada ya kuondoka Leicester City ingekuwa mwisho wake na asingeng’ara akiwa na Chelsea. 
 
Lakini msimu huu anaonekana anaenda tena kutengeneza historia mpya kwa kuwapa ubingwa Chelsea.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...