Skip to main content

Tanzania kuisaidia Kenya na madaktari.!

Serikali ya Tanzania imekubali ombi la Kenya la kuisaidia nchi hiyo na madaktari 500 watakaosaidia kukabiliana na tatizo la uhaba wa madaktari katika vituo vyake vya tiba kufuatia kutokea kwa mgomo wa madaktari nchini humo.

Rais wa taifa hilo John Pombe Magufuli amekubali kutoa madaktari hao baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa Kenya wa maafisa wa afya uliotumwa kwake na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.

Kiongozi huyo amesema kuwa Tanzania imekubali ombi hilo kwa kuwa Kenya ni jirani ,ndugu na rafiki wa kweli wa Tanzania na amemtaka waziri wa afya nchini humo Ummy Mwalimu kuharakisha mchakato huo ili maafisa hao waelekee Kenya kutekeleza jukumu hilo.

Serikali ya Tanzania imekubali ombi la Kenya la kuisaidia nchi hiyo na madaktari 500 watakaosaidia kukabiliana na tatizo la uhaba wa madaktari katika vituo vyake vya tiba kufuatia kutokea kwa mgomo wa madaktari nchini humo.

Rais wa taifa hilo John Pombe Magufuli amekubali kutoa madaktari hao baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa Kenya wa maafisa wa afya uliotumwa kwake na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
 
Kiongozi huyo amesema kuwa Tanzania imekubali ombi hilo kwa kuwa Kenya ni jirani ,ndugu na rafiki wa kweli wa Tanzania na amemtaka waziri wa afya nchini humo Ummy Mwalimu kuharakisha mchakato huo ili maafisa hao waelekee Kenya kutekeleza jukumu hilo.

''Matatizo ya Kenya ni matatizo ya Tanzania, tutawapatia madaktari hao 500 wakatoe huduma kwa ndugu zetu waliopo Kenya na kwa kuwa mumenihakikishia kuwa madaktari wangu watalipwa mishahara inavyostahili, kufanya kazi katika mazingira mazuri mbali na kuwapa nyumba za kuishi, sina tatizo naamini mambo yatakuwa mazuri'', alisema Magufuli.

Waziri wa afya wa Kenya Dkt. Cleopa Mailu ambaye aliongoza ujumbe huo alimweleza rais Magufuli kwamba baada ya mgomo wa madaktari pamoja na uamuzi wa taifa hilo kugatua madaraka katika sekta ya afya imebainika kuwa taifa hilo lina uhaba mkubwa wa madaktari ambao hauwezi kumalizwa kwa kutegemea madaktari wanaosomeshwa nchini humo bali kupata madaktari kutoka nje.

Mheshimiwa Jack Ranguma ambaye alikuwa katika ujumbe huo wa Kenya amesema kuwa Kenya itawalipa madaktari hao kwa stahili zote ikiwa ni mishahara na nyumba za kuishi.

Naye waziri wa afya na ustawi wa jamii nchini Tanzania Ummy Mwalimu amesema kuwa wizara yake iko tayari kutoa madaktari hao haraka iwezekananvyo akisema kuwa Tanzania ina madaktari wengi wazuri ambao wamehitimu lakini hawajapata ajira, huku wengine wakimaliza mikataba yao ya kazi wakiwa na uwezo wa kufanya kazi.

''Kwa hiyo nitoe wito kwa madaktari wote nchini Tanzania ambao hawapo katika utumishi wa umma, hawapo katika hospitali teule na ambao hawapo katika hospitali za mashirika yasiokuwa ya serikali wanaolipwa na serikali waombe nafasi hizi''

''Vigezo tunavyaongalia ni kwanza awe amemaliza mafunzo ya vitendo yani Internship, pili awe amesajiliwa na baraza la madaktari la Tanganyika. Kwa hiyo leo hii tunatoa tangazo na tumefurahi sana kwa sababu tuna madaktari wa kutosha ndani ya nchi na tunaweza kuwapeleka Kenya'',alisema muheshimiwa Ummy.BBC

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...