Skip to main content

KADI ZA TIKETI ZA ELEKTRONIKI KUTOLEWA BUREEE KABISA, WAZIRI NAPE ALIZUNGUMZIA ZOEZI

Kadi za kilektroniki kwa ajili ya kuingia uwanjani zitakuwa zikitolewa bure.

Hii ni ni baada ya ya hivi karibuni serikali kufunga mashine za kielektroniki katika Uwanja wa Taifa, kadi kwa ajili ya kuingilia uwanjani humo zitatolewa bure.

Serikali iliamua kufunga mashine hizo katika uwanja huo ili kuondokana na mfumo wa zamani wa kutumia tiketi za kawaida kwa lengo la kulinda mapato yake uwanjani hapo ambayo kwa kiasi kikubwa yalikuwa yakiishia mifukoni mwa wajanja wachache.


Akizungumza katika semina elekezi ya jinsi ya kutumia mfumo huo mpya wa kuingia uwanjani humo uliozinduliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, Meneja Miradi wa Kampuni ya Selcom ambayo ndiyo iliyopewa jukumu la kusimamia mfumo huo, Gallus Runyeta amesema kuwa kadi zitakazokuwa zikitumika katika mfumo huo zitatolewa bure.

Amesema kadi hizo zitaanza kutolewa hivi karibuni ambapo kutakuwa na mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaofanyika katika uwanja huo ambao serikali kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) watauandaa kabla ya mchezo wa Yanga na Simba.

“Kadi zinapatikana kwa mawakala wetu (wa Selcom) waliopo kila sehemu. Lazima ununue tiketi halafu unapewa kadi bure,” alisema Runyeta.

Akizungumzia jinsi ya kuitumia kadi hiyo, Runyeta amesema: “Utajisajili kwa kupiga *150*50# halafu ni lazima uiwekee pesa kwa Airtel au M-Pesa. Kiwango cha chini cha kuongeza salio ni Sh 1,000.

“Unaweza ukanunua mechi moja kwa kuandika tarehe na mchezo husika au ukachagua baadhi ya mechi au ukanunua mechi zote za msimu za timu unayoipenda.

“Unapokwenda kuingia uwanjani, utaweka kadi yako kwenye alama husika na mlango utafunguka wenyewe. Ukishaangalia mechi uliyoinunua, hauwezi kesho yake ukaenda kutazama mechi nyingine ambayo hujailipia. Kadi itasoma kwenye mechi zilizolipiwa tu. Ukiingia uwanjani hauwezi ukatoka halafu ukarudi kwa tiketi ileile. 

Tunawashauri watu wawe wananunua tiketi mapema ili kuepusha usumbufu na msongamano milangoni. Unaweza ukanunua siku nyingi kabla.”


Ameongeza: “Mbali na kadi hizo kuzitumia uwanjani, pia aliyenayo anaweza kuitumia kwa matumizi mengine kama vile kuhifadhi na kutoa fedha kwa wakala, lakini pia inamwezesha mtu huyo kulipia bidhaa na huduma mbalimbali bila kuwa na fedha mfukoni.”

Wakati huohuo, Nnauye amemuagiza Naibu Mkurugenzi wa Michezo Tanzania, Nkenyenge Alex kuhakikisha anaandaa sera ya michezo nchini mapema iwezekanavyo mpaka kufikia mwezi Septemba iwe tayari.

Amesema lengo kubwa la kufanya hivyo ni kutaka kuleta mapinduzi makubwa ya michezo hapa nchini kwani sera iliyopo hivi sasa imeshapitwa na wakati.

“Nimemwambia nataka mpaka kufikia Septemba sera hiyo iwe tayari, kama atashindwa kufanya hivyo, basi akatafute sehemu nyingine ya kufanya kazi pamoja na wenzake wote,” amesema Nnauye.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...