Skip to main content

WABUNGE YANGA, SIMBA WAUNGANA KUCHANGIA WALIOKUTWA NA MAAFA YA TETEMEKO LA KAGERA

Wabunge wapenzi wa Simba wanatarajia kuumana wikiendi hii, ikiwa ni mechi mahsusi kwa ajili ya kuchangisha fedha za kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni huko mkoani Kagera.

Mbali na mechi hiyo pia kutakuwa na mechi za ufunguzi baina ya Bongo Muvi dhidi ya Bongo Fleva, pia kutakuwa na mechi ya netiboli itakayoikutanisha timu ya bunge dhidi ya ile ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), mechi zote hizo zitapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Mbunge wa Sengerema na Mwenyekiti wa Bunge SC, William Ngeleja ameweka wazi kuwa licha ya wabunge hao kuchangia kiasi cha Sh milioni 85 kupitia posho zao wakiwa bungeni lakini bado wameona kuna msaada zaidi unahitajika kwa ajili ya angalau kurejesha hali ya maisha ya awali ya Kagera ndiyo maana kumeandaliwa mechi hizo.

“Lengo letu ni kukusanya fedha za kuwasaidia ndugu zetu wa kule Kagera, angalau warejewe na hali waliyokuwa nayo awali, tangu awali kule bungeni kupitia posho zetu tulishachanga milioni 85 lakini tunahitaji kuongeza zaidi misaada kwao ndiyo maana tumeandaa mechi hii ili kila Mtanzania kupitia kiingilio alichonacho naye ashiriki kuwakomboa ndugu zetu hawa.

“Vikosi vitakuwa vikali kwa ajili ya kutoa burudani ya kutosha, huku kwetu Simba tutakuwa na Kassim Majaliwa, Hamis Kigwangwala, Kaizer Makame na wengine. Kule Yanga nao watakuwa na Ridhiwani Kikwete, Anthony Mavunde, Mwigulu Nchemba na wengine wengi.

“Bongo Muvi wao watakuwa na kina Ray Kigosi, JB, Muhogo Mchungu, Dk. Cheni na wengine, lakini Bongo Fleva wao watakuwa na kina Tundaman, Ali Kiba, Diamond, KR Mullah na wengine. Kuhusu mgeni rasmi, tunakamilisha taratibu na muda si mrefu tutamtangaza,” alisema Ngeleja ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Sengerema.

Tayari viingilio vya mechi hiyo itakayopigwa Jumapili hii vimeshawekwa wazi ambapo Sh 3,000 itakuwa kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, Sh 10,000 na 15,000 itakuwa kwa ajili ya viti vya rangi ya machungwa huku Sh 50,000, 100,000 na 200,000 ikiwa ni kwa V.I.P C, B na A.

Lakini kwa viti 50 pekee maalum vitakavyokuwa karibu na mgeni rasmi wa mechi hiyo ambaye atatajwa baadaye, kila kimoja kitalilipiwa Sh 1,000,000.

  Chanzo saleh jembe.

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...