Skip to main content

Aliyecopy hotuba ya Obama na kumpa Rais Buhari…Kufukuzwa kazi



Wiki iliyopita Ikulu ya Nigeria kupitia kwa muandishi wa hotuba za Rais, iliingia kwenye skendo ya kunakili hotuba ya Rais Barack Obama na kumpa Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari ambaye aliisoma kama ilivyo bila kujua, mpaka wapinzani walipoanzisha mzozo juu ya suala hilo.
Official responsible for Plagiarism of Obama's Speech to be sacked
Sehemu ya hotuba ya Rais Buhari iliyonakiliwa kutoka kwenye hotuba ya Rais Barack Obama aliyoitoa mwaka 2008 inasema “Change Begins With Me” Mabadiliko Huanza Na Mimi, ikifahamika kwa jina la Hotuba ya Ushindi.
Ikulu ya Nigeria imeomba radhi juu ya aibu iliyomkuta Rais wa nchi hiyo na kuahidi kumchukulia hatua kali za kinidhamu muandishi aliyesababisha.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Trust limesema kuwa kiongozi huyo msaidizi wa idara ya mawasiliano ya Rais, ataondolewa kazini kutokana na uzembe alioufanya. Muda mfupi tangu kutokea tatizo hilo, Taasisi ya Rais kupitia idara ya mawasiliano kwa Umma imeripoti kuwa itaweka software itakayokuwa ikigundua kama hotuba zote za Rais zimenakiliwa kutoka sehemu nyingine. 
Msemaji wa Serikali ya Nigeria amesema >>>Tumepanga kuchukua hatua ya kuweka kifaa kitakachokuwa na uwezo wa kukagua na kugundua kama hotuba za Rais zimenakiliwa kutoka sehemu nyingine kabla ya kumkabidhi Rais,”
Kitendo cha Hotuba ya Rais Buhari kunakiliwa kutoka kwenye Hotuba za Rais Obama, kimewafanya vyama vya upinzani nchini humo kusema kuwa ipo siku Rais huyo atasaini nakala za kujiuzulu bila kujua kutokana na kutozikagua kabla ya kuzisoma.Chanzo MIlad Ayo

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...