Skip to main content

YANGA WANAHITAJI ALAMA TATU(3) TU KUTANGAZA UBINGWA-VPL .!

Yanga wanahitaji pointi tatu pekee ili kutangaza ubingwa wao katika msimu huu kabla ya mechi za mwisho za ligi Mei 20, 2017. 

Baada ya ushindi wa jana Mei 13, 2017  wa magoli 2-1 dhidi ya Mbeya City, Yanga imefikisha pointi 65 sawa na Simba na inaongoza ligi kutoka na wastani wa magoli ya kufunga na kufungwa.

Kama watapata pointi tatu kwenye mechi yao ya kiporo itakayochezwaJumanne dhidi ya Toto Africans zitaifanya Yanga kutangaza ubingwa katika msimu huu 2016/2017,

 kwa sababu watafikisha pointi 68 ambapo hata Simba ikishinda mechi yake ya mwisho dhidi ya Mwadui haitasaidia kwa sababu watafikisha pointi 68 sawa na Yanga lakini watahukumiwa na tofauti ya magoli.

Yanga walianza kupata goli la kwanza dakika ya 7 kipindi cha kwanza mfungaji akiwa ni Simon Msuva ambaye aliunganisha kwa kichwa mpira wa krosi ya Hassan Hamisi Ramadhani ‘Kessy’. 

Mbeya City walisawazisha goli hilo dakika ya 58 kupitia kwa Haruna Shamte baada ya kazi kubwa kufanywa na Ditram Nchimbi kisha kumaliziwa na Shamte.

Obrey Chirwa ameendelea kuonesha ubora wake kwenye ligi ya Bongo baada ya kuifungia Yanga goli muhimu ambalo limeamua mchezo wa leo na kuirejesha timu yake kwenye nafasi ya kwanza ya msimamo wa VPL.

Chirwa amefunga goli hilo akiunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Juma Abdul.

Yanga inaizidi Simba kwa wastani wa magoli 11, Yanga ina wastani wa magoli 43 wakati Simba wao wanawastani wa magoli 32 hadi sasa.

Simba imebakiza mechi moja ili imalize mechi zake zote (30) za ligi kuu Tanzania bara kwa msimu huu, endapo watashinda mechi hiyo watafikisha pointi 68,

 lakini Yanga wamebakiza mechi mbili (Yanga vs Toto Africans na Mbao FC vs Yanga) wakishinda mechi yao ya dhidi ya Toto watatangazwa rasmi kama mabingwa wapya wa VPL matokeo tofauti na ushindi, yatapelekea bingwa kujulikana siku ya mwisho ya mechi za kufungia ligi.

Ikiwa Simba itafungwa kwenye mchezo wake wa mwisho dhidi ya Mwadui basi Yanga watakuwa mabingwa hata kama watapoteza mechi zao zote mbili za mwisho.

Ushindi wa Yanga kwa jana ni sawa na kulipa kisasi kwa Mbeya City kwa sababu mechi ya mzunguko wa kwanza iliyochezwa November 2, 2016 Mbeya City walishinda kwa magoli 2-1 mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Matokeo mengine ya mechi zilizochezwa jana
Kagera Sugar 2-1 Mbao FC
JKT Ruvu 0-1 Majimaji
Tanzania Prisons 2-1 Ndanda FC
Mtibwa Sugar 4 -2 Mwadui FC

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...