Skip to main content

KING-LEO MESSI AAPA KUSALIA BARCELONA HADI TAMATI.! Bofya picha hii

Lionel Messi alifunga magoli manne katika mechi ya fainali ya Copa del Rey, na kuwa mchezaji wa kwanza tangu mchezaji wa Athletic Bilbao Telmo Zarra kufanya hivyo mwaka 1950.
Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi amesema angependa kusalia na klabu yake kwa siku zilizosalia katika taaluma yake.
''Ni kitu ambacho nimekuwa nikikitazamia na ni kitu nilichokuwa nikikitaka," alisema.
Kiungo huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na Barcelona akiwa na umri wa miaka 13, akashiriki mechi yake ya kwanza akiwa na umri wa miaka 17 na amefunga zaidi ya magoli 500 akiwa na klabu hiyo.
Messi ameshinda taji La liga mara nane, Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mara nne na tuzo mchezaji bora duniani Ballon d'Or mara tano.
Msimu uliopita chini ya kocha Luis Enrique, Barcelona walikuwa katika nafasi ya pili kwa ligi ya La Liga, alama tatu chini ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Real Madrid.
Walishindwa 3-0 katika robo fainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Juventus.
Enrique alitangaza mwezi Machi, kwamba angeiaga klabu hiyo baada ya mkataba wake wa miaka mitatu kumalizika, mechi yake ya mwisho ilikuwa ni pale Barca walipojinyakulia kombe la Copa Del Rey .
Messi alifunga bao la ufunguzi walipoichapa Alaves mabao 3-0 na kupata ushindi.
Messi ambaye alikuwa wa pili nyuma ya mshambuliaji wa Real, Cristiano Ronaldo katika tuzo ya Ballon d'Or, aliuambia mtandao wa Barcelona lengo lake ni ''kujaribu kuimarika kila msimu hadi mwisho, na hilo ndilo lengo langu la msimu ujao.''  BBC 

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...