Skip to main content

Duterte asema Obama anaweza 'kwenda jehanamu'............//

Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte amerejelea tena shutuma zake dhidi ya Rais Obama na viongozi wengine wa nchi za Magharibi wanaopinga mpango wake wa kupambana na walanguzi wa dawa za kulevya.
Kiongozi huyo amesema Bw Obama anaweza "kwenda jehanamu".
Umoja wa Ulaya, ambao pia umemkosoa Bw Duterte, unaweza "kuchagua kwenda eneo la kutakasia dhambi ndogo, kwa sababu jehanamu kumejaa", amesema.
Watu karibu 3,000 wameuawa tangu kiongozi huyo alipoingia madarakani mwezi Juni.
Watu wanaoshukiwa kulangua mihadarati au kuwa waraibu wa dawa hizo wamekuwa wakiuawa na maafisa wa polisi na magenge yanayoungwa mkono na serikali.
Bw Duterte amesema Urusi na China wako tayari kuwa washirika wake.
Image copyright AP
Image caption Bw Duterte
Wanajeshi wa Ufilipino na Marekani kwa sasa wanafanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi lakini Bw Duterte amesema mazoezi hayo hayana manufaa kwa raia wa Ufilipino.
Msemaji wa ikulu ya White House Josh Earnest amesema Washington kufikia sasa haijapokea ombi lolote rasmi kutoka kwa Ufilipino kufanyia marekebisho mikataba ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Akiwahutubia maafisa wa serikali na wafanyabiashara, Bw Duterte amesema amesikitishwa sana na Marekani kwa kukosoa mbinu za Ufilipino za kukabiliana na mihadarati.
Ameeleza Marekani kama mshirika asiye wa kutegemewa.
"Badala ya kutusaidia, wizara ya mambo ya nje (ya Marekani) ndio wa kwanza kutukosoa, kwa hivyo wanaweza kwenda jehanamu, Bw Obama, unaweza kwenda jehanamu."
Baadaye Jumanne, alitahadharisha kwamba: "Mwishowe huenda, nikiwa bado uongozini, nikajitenga na Marekani. Heri kwenda kwa Urusi au Uchina."
Aidha, Bw Duterte amefichua kwamba Marekani imekataa kiuzia silaha serikali yake lakini akaongeza kwamba watazinunua kwingine.
"Iwapo hamtaki kuuza silaha, nitaenda Urusi. Niliwatuma majenerali Urusi na Urusi walisema, 'Msiwe na wasiwasi, tuna kila kitu mnachohitaji, tutawapa'.
"Kuhusu China, walisema, 'Njooni na mtie saini na kila kitu kitafikishwa kwenu'," Rais Duterte amesema.
Ufilipino ilikuwa koloni ya Marekani na imekuwa mshirika mkuu Asia mashariki.
Image copyright Associated Press
Image caption Wanaharakati waliandamana nje ya ubalozi wa Markani, Manila adhidi ya ushirikiano wa kijeshi kati ya Ufilipino na Marekani
Image copyright AFP/Getty Images
Image caption Zaidi ya wanajeshi 1,100 wa Marekani wanashiriki mazoezi ya pamoja na wanajeshi wa Ufilipino. Huyu hapa ni kamanda mkuu wa jeshi la wanamaji la Ufilipino Meja Jenerali Andre Costales akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa mazoezi ya sasa Manila
Wanajeshi 1,100 wa Marekani na 400 wa Ufilipino wanashriiki mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi ambayo yataendelea kwa siku nane.
Uhusiano baina ya Marekani na Ufilipino ulidorora mwezi uliopita baada ya Rais Duterte kuonekana kumtusi Rais Obama.BBC

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...