Skip to main content

KUELEKEA MCHEZO WA REAL VS UNITED, HIZI NDIO TAKWIMU NA RECORDS ZA UEFA SUPER CUP.

Msimu mpya wa soka barani Ulaya unatarajiwa kuanza rasmi leo wakati utakapopigwa mtanange utakaowakutanisha wababe wa ulaya msimu uliopita. Mabingwa wa Champions League Real Madrid na mabingwa wa Europa Cup Manchester United.

Mchezo huu utapigwa nchini Macedonia mashariki mwa bara la ulaya, kuanzia majira ya 9:45 usiku.
Mchezo huu unakutanisha miamba mikubwa ya soka barani ulaya siku chache baada ya kukutana nchini Marekani katika mechi za maandalizi ya msimu mpya. 


Cristiano Ronaldo amerejea mazoezini wiki iliyopita na leo ametajwa katika kikosi kinachosafiro kuelekea Macedonia kwa ajili ya mchezo huo, United watamkosa Eric Bailly pamoja na Phil Jones wenye adhabu za kufungiwa mechi kutokana na makosa ambayo waliyatenda msimu uliopita.


Kwa kuanzia kuuchambua mchezo huu tuanze kuangalia takwimu mbalimbali zinazohusisha mchezo wa UEFA Super Cup tangu ulipoanzishwa kuchezwa mnamo mwaka 1973.

Champions League vs UEFA Cup Winners
• Mabingwa wa Champions League wameshinda kombe hili mara 22 kati ya mara 41.
• Mabingwa wa UEFA Cup/UEFA Europa League wameshinda kombe hili mara 7 kati ya 17 tangu lilipokufa kombe la Washindi (UEFA Cup Winners' Cup.)

Mataifa yaliyoshinda mara nyingi
13: Spain 🇪🇸 wameshinda kombe hili mara 13 kupitia vilabu vyao (Barcelona 5, Real Madrid 3, Valencia 2, Atlético Madrid 2, Sevilla 1)

9: Italy 🇮🇹 wameshinda Super Cup mara 9 kupitia vilabu vyao (AC Milan 5, Juventus 2, Lazio 1, Parma 1)
7: England wanafuatia kwa kushinda mara 7 (Liverpool 3, Aston Villa 1, Chelsea 1, Manchester United 1, Nottingham Forest 1)

Vilabu vilivyoshinda UEFA Super Cup mara nyingi
5: AC Milan, Barcelona
3: Liverpool, Real Madrid
2: Ajax, Anderlecht, Atlético Madrid, Juventus, Valencia

Mchezaji aliyeshinda Super Cup Mara nyingi
4= Dani Alves (Sevilla 2006, Barcelona 2009, 2011, 2015)
4= Paolo Maldini (AC Milan 1989, 1990, 1994, 2003)


Kocha aliyeshinda mara nyingi
3= Carlo Ancelotti (AC Milan 2003, 2007, Real Madrid 2014)
3= Josep Guardiola (Barcelona 2009, 2011, Bayern München 2013)


Nchi zilizoshiriki mchezo wa Super Cup mara nyingi
25: Spain wameshiriki mara 25 kupitia vilabu vya (Barcelona 9, Real Madrid 6, Sevilla 5, Valencia 2, Atlético Madrid 2, Real Zaragoza 1)

16: Waingereza 🇬🇧 wameshiriki mara 16 kupitia vilabu vya (Liverpool 5, Manchester United 4, Chelsea 3, Nottingham Forest 2, Arsenal 1, Aston Villa 1)
13: Italy mara 13 (AC Milan 7, Juventus 2, Internazionale Milano 1, Parma 1, Lazio 1, Sampdoria 1)
Vilabu vilivyoshiriki mara nyingi
9: Barcelona
7: AC Milan
6: Real Madrid
5: Liverpool, Sevilla
4: Bayern München, Porto, Manchester United

Mchezo uliokuwa na idadi kubwa ya magoli : 2015, Barcelona 5-4 Sevilla
Ushindi mkubwa zaidi *: 2006, Sevilla 3-0 Barcelona, na mtanange wa 2012 kati ya Atlético Madrid 4-1 Chelsea
Rekodi binafsi
Goli la haraka zaidi: Éver Banega (Dakika 3 – 2015: Barcelona 5-4 Sevilla)

Waliofunga Hat-tricks: Radamel Falcao (2012, Atlético Madrid v Chelsea) na Terry McDermott (1977, Liverpool v Hamburg)

Waliofunga magoli ya kujifunga: Patrick Paauwe alijifunga goli pekee katika historia ya Super Cup kwenye mchezo wa kipigo cha Feyenoord cha mabao 3-1 kutoka kwa Real Madrid mwaka 2002.

Waliopata kadi nyekundu: Wachezaji wanne wameshapata kadi nyekundu kwenye mchezo wa Super Cup – Paul Scholes (2008, United), Rolando na Fredy Guarín (2011, Porto) na Thimothée Kolodziejczak (Sevilla, 2016).

Wachezaji waliocheza mechi nyingi za UEFA Super Cup **
8: Alessandro Costacurta (AC Milan), Roberto Donadoni (AC Milan)
7: Paolo Maldini (AC Milan), Daniele Massaro (AC Milan), Mauro Tassotti (AC Milan)
6: Franco Baresi (AC Milan), Arie Haan (Ajax, Anderlecht)
5: Dani Alves (Sevilla, Barcelona), Marcel Desailly (AC Milan, Chelsea), Albert Ferrer (Barcelona, Chelsea), Ronald Koeman (PSV Eindhoven, Barcelona), Attilio Lombardo (Sampdoria, Juventus, Lazio), Phil Neal (Liverpool)


Wafungaji bora wa UEFA Super Cup
3: Oleh Blokhin (Dynamo Kyiv), Radamel Falcao (Atlético Madrid), Arie Haan (Ajax, Anderlecht), Terry McDermott (Liverpool), Lionel Messi (Barcelona), Gerd Müller (Bayern München), Rob Rensenbrink (Anderlecht), François Van der Elst (Anderlecht

**UEFA Super Cup ulikuwa unachezwa kwa mfumo wa mechi za nyumbani na ugenini kuanzia mwaka 1973 mpaka 1997. DAUDA

Comments

Popular posts from this blog

Fedha za nchi 7 kutoka Afrika ambazo zina thamani zaidi.!

Kuna baadhi ya nchi nyingi barani Afrika ambazo fedha zake zimekuwa maarufu kutokana na uchumi wake kuwa mkubwa na zipo nchi nyingine ambazo pamoja na kuwa na watu wengi kwenye miji yao lakini bado fedha inakosa thamani. Nguvu au thamani ya fedha inaweza kupimwa kwa uwezo wa kununua, kuonyesha jinsi uchumi wa nchi husika unavyokuwa kwa kulinganisha na nchi nyingine duniani.  Leo April 1 2017 nakuletea list ya nchi saba kutoka Afrika ambazo fedha zake zina nguvu na thamani kubwa kuliko nchi nyingine. 7: Rand – Afrika Kusini (1$=14) Ukiiweka kando Nigeria nchi nyingine ambayo uchumi wake una nguvu ni Afrika Kusini ambapo hata hivyo kutokana na mgogoro wa kiuchumi kimataifa, thamani ya Rand imekuwa ikiporomoka thamani yake kutokana na kupanda kwa Dolla ambapo sasa unaweza ukabadilisha Dola moja kwa Rand 14. 6: Pula – Botswana (1$ = 10.8) Pula ndiyo fedha ambayo inatumika katika nchi ya Botswana ambayo uchumi wake mkubwa unatokana na mapato yatokana...

TETESI ZA SOKA MAJUU LEO JUMA PILI JULAI 16 2017.!Bofya picha hii kutazama tetesi zote.

Real Madrid wanafikiria kumuuza mshambuliaji Gareth Bale, 27, ili kupata fedha za kumnunua Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Sunday Express) Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anaamini Kylian Mbappe atabakia Monaco kwa msimu mmoja zaidi. (Sun on Sunday) Dau la Chelsea la pauni milioni 88 la kumtaka mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 29, limekataliwa. (Tuttosport) Kuna wasiwasi kuhusu hatma ya meneja wa Chelsea Antonio Conte, 47, baada ya mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua. (Sun on Sunday) Liverpool wanatarajiwa kupanda dau jipya kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22 wiki ijayo, baada ya dau la pauni milioni 57 kukataliwa. (Sunday Mirror) Kumekuwa na wasiwasi zaidi kuhusiana na mustakbali wa Alexis Sanchez, 28, baada ya kusema anataka kucheza Klabu Bingwa Ulaya. (ESPN Manchester City wanaongeza juhudi zao za kutaka kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22, kwa pauni milioni 50 hii ni baada ya Tottenham kukataa kuwauzia Da...

Matumizi ya silaha za sumu Syria kuchunguzwa.! Bofya picha hii kupata story nzima.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mashambulizi yanayotuhumiwa kuwa ya silaha za sumu yaliofanyika nchini Syria hapo Jumanne yanapaswa kuchunguzwa. Kauli ya Guterres inakuja wakati kundi linalofuatilia hali ya Syria likisema idadi ya vifo kutokana na mashambulio hayo ya Jumanne katika mji wa kaskazini imeongezeka na kufikia 72, na wanaharakati pia wameripoti kurudiwa kwa mashambulizi ya anga katika mji huo. Guteress amewaambia waandishi wa habari leo hii katika mkutano wa wafadhili wa Syria unaofanyika Brusels kwamba anataraji wakati huu utaweza kuimarisha uwezo wa wale ambao wana wajibu katika hali hiyo. Amesema matukio hayo ya kutisha yanaonyesha uhalifu wa kivita ukiendelea kutendeka nchini Syria na kwamba sheria ya kimataifa inaendelea kukiukwa mara kwa mara.Ameongeza kusema ana imani kwamba Baraza la Usalama litatimiza wajibu wake wakati litakapokutana baadae leo hii. Baraza la Usalama kujadili mashambulizi hayo Marekani, Ufarans...